Mtu Mrefu zaidi Tanzania, Bw. Julius Charles ametembelea banda la Mfuko wa Misitu Tanzania lililopo katika viwanja vya maonesho ya Nanenae vya John Mwakangale Jijini Mbeya. Bw. Julius Charles amepatiwa maelezo kuhusu fursa za uwezeshaji unaotolewa na Mfuko ikiwemo namna ya kuomba ruzuku inayotolewa na Mfuko. Picha inaonesha Afisa Miradi wa Mfuko wa Misitu Tanzania, Bw. Juma Ally na Afisa Tehama Bw. Kisanga wakimkabidhi Bw. Julius Vipeperushi muhimu za Mfuko wa Misitu Tanzania.