Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) ni Mfuko Umma unaojishughulisha na uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa njia ya kutoa ruzuku. Mfuko umeshiriki kwenye maonesho ya mifuko na program za uwezeshaji wananchi kiuchumi yaliyofanyika kuanzia tarehe 21 - 27 Mei, 2023 mjini Kigoma.
Kwenye picha ni Bw. Juma Ally (Afisa Miradi Kutoka TaFF) akitoa maelezo kwa Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo juu ya shughuli za Mfuko na kuelezea utaratibu wa utoaji ruzuku kuwawezesha wananchi kiuchumi.
Kwa Picha Zaidi Tembelea: https://www.mfukowamisitu.go.tz/index.php/newsroom/gallery/taff-washiriki-maonesho-ya-sita-ya-mifuko-na-programu-za-uwezeshaji-2023-kigoma