Top
  • The United Republic of Tanzania

    Ministry of Natural Resources and Tourism

    Tanzania Forest Fund-TaFF

NEEC YATAMBUA MCHANGO NA UTENDAJI WA TaFF, YAIPATIA TUZO.

Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) imeshika nafasi ya pili katika  tuzo ya utendaji bora na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kama sehemu ya  mchango wake katika uwezeshaji wananchi kiuchumi na utendaji bora wa mfuko huo. 

Kabla ya kutoa tuzo hizo kwenye kongamano la Saba la uwezeshaji wananchi kiuchumi, Jijini Dodoma,  Waziri Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) amezipongeza Taasisi na Sekta zote binafsi zinazo jishughulisha na uboreshaji wa Maisha ya wananchi kiuchumi na kuwa huko nikuunga mkono kwa vitendo juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea wananchi maendeleo. 

Waziri Mkuu Majaliwa, ametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya Maliasili na Utalii ili kujiendeleza kiuchumi na kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla.

Akizungumza  baada ya kupokea tuzo hiyo,  Katibu Tawala Mfuko wa Misitu Tanzania, Dkt. Tuli Salum Msuya ameishukuru NEEC kwa kutambua mchango wa TaFF katika kuwezesha wananchi kiuchumi na kutambua utendaji bora wa Mfuko huu hali iliyopelekea kupewa tuzo.

Dkt. Msuya ameendelea kusema  kuwa  tuzo hiyo ni kichocheo cha utendaji kazi zaidi kwa  Mfuko huo ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika  na fursa zilizopo katika sekta ya Misitu na  kuchangia zaidi katika  pato Taifa.

Aidha Dkt. Msuya ameongeza kuwa TaFF hutoa ruzuku kwa lengo la kuwezesha miradi ya kuboresha uhifadhi, uendelezaji na usimamizi wa rasilimali misitu hapa nchini.

Wafanyakazi wa Mfuko wa Misitu Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kupokea na kushangilia ushindi wa pili wa utendaji bora kutoka Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) katika chumba cha mikutano ofisi za TaFF Dodoma. Kwenye picha ni Katibu Tawala aliyevalia koti jeupe akiongoza timu ya ushindi.

Kwa picha zaidi tembelea: https://www.mfukowamisitu.go.tz/index.php/resources/photos